.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumanne, 15 Septemba 2015

BASI LA METRO LAPATA AJALI MKOANI TANGA, ABIRIA 5 WAMEFARIKI NA WENGINE 39 WAMEJERUHIWA

Basi la Metro lililokuwa linatoka jijini Dar es Salaam kuelekea wilayani Rombo mkoani Kilimanjaro, limepinduka katika eneo la Manga, wilaya ya Handeni mkoani Tanga. 

Katika ajali hiyo, watu 5 wamefariki dunia na wengine 39 wamejeruhiwa na kukimbizwa katika hospitali kwa matibabu. 

Kamanda wa Polisi mkoa wa Tanga, Zuberi Mwombeji amethibitisha kutokea kwa ajali hiyo, ambapo amesema chanzo cha ajali ni mwendo kasi wa dereva wa basi hilo, ambaye alishindwa kulimudu basi hilo wakati alipofika katika eneo lenye kona na hivyo kusababisha kupinduka. 

Kamanda Mwombeji amesema baada ya ajali hiyo, dereva alikimbia na jeshi la polisi linaendelea kumsaka ili aweze kufikishwa katika vyombo vya sheria.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni