Muigizaji filamu Emma
Thompson amedai kuwa Uingereza haichukui kiasi kikubwa cha wakimbizi
kutoka mataifa ya Ulaya kutokana na umma wake kuwa ni wabaguzi.
Mshindi huyo wa tuzo ya
Oscar, amesema namna Uingereza inavyoshughulikia mgogoro wa wahamiaji
ni aibu, na kusema kuna nafasi ya kutosha kuhifadhi maelfu ya
wakimbizi.
Hatua hiyo ya muigizaji
huyo nyota imekuja huku kukiwa na shinikizo kwa serikali ya Uingereza
kutoa hifadhi kwa familia zaidi za wakimbizi wa Syria wanaokimbilia
mataifa ya Ulaya.


Hakuna maoni :
Chapisha Maoni