.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumatano, 16 Septemba 2015

MWILI WA WAZIRI WA MAMBO YA NDANI WA UGANDA WAWASILI ENTEBBE

Mwili wa Waziri wa Mambo ya Ndani wa Uganda, Jenerali Aronda Nyakairima aliyefariki dunia nje ya nchi umewasili kwa ndege leo mchana ukitokea Dubai.

Mwili Aronda ambaye aliwahi pia kuwa Mkuu wa Jeshi la Uganda umewasili majira ya saa saba na nusu mchana na kupokelewa na mkewe, watoto wake, ndugu wa karibu, viongozi wa serikali na wanajeshi wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi Uganda.

Marehemu Jenerali Aronda Nyakairima ambaye alikuwa ni mwanajeshi mwenye ujuzi wa hali ya juu, alifariki dunia jumamosi iliyopita akiwa njiani kurejea Uganda.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni