.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Alhamisi, 3 Septemba 2015

POLISI WAMKAMATA MTUHUMIWA WA MAUAJI HOTEL A SQUARE BELMONT

Hatimaye mtuhumiwa wa mauaji ya mfanyabiashara wa mabegi soko kuu Jijini Arusha, Alfred Kimbaa (18), maarufu kwa jina la Mandela aliyekutwa amechinjwa katika hotel ya A. Square Belmont, huku mwili wake ukiwa hauna baadhi ya viungo kama kichwa, sehemu za siri, viganja
vya mikono yake na matiti,amepatikana.

Mtuhumiwa huyo amefahamika kwa jina la Eligius Edward Lyatuu (31), ambaye ni mwanafunzi wa mwaka wa tano, katika chuo cha Falsafa cha Kanisa Katoliki, kilichopo Segerea Jijini Dar es Salaam.

Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake, Kamanda wa Polisi Mkoani Arusha, Liberatus Sabas, amesema kuwa mtuhumiwa huo alifanya mauaji hayo, Agosti 30 mwaka huu, katika chumba cha hotel hiyo na kasha kutoweka na viungo hivyo.

Sabas amesema baada ya uchunguzi wao kwa kushirikiana na wananchi wenye mapenzi mema na jeshi hilo, Septemba Mosi, walimkamata mtuhumiwa huyo, eneo la Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) na baadaye alikwenda kuonyesha viungo hivyo, alikoficha, pembeni mwa mto Mission uliopo Usa river Wilayani Arumeru.

Amesema chanzo cha mauaji hayo ni ugomvi kati yao yaani marehemu na mtuhumiwa, ambao hakutaja kwa madai ni moja ya vielelezo mahakamani.

Kamanda Sabas amesema mtuhumiwa alifika Arusha akitokea chuoni Dar es Salaam na kuishi nyumbani kwa marehemu Mianzini na mtuhumiwa ni kaka wa mwenye duka alilokuwa akiuza marehemu.

Amesema viungo hivyo vimeunganishwa katika mwili wa marehemu na uchunguzi umefanyika jana, ili ndugu zake wachukue kwa mazishi na baadaye mtuhumiwa atafikishwa mahakamani wakati wowote.

Awali mwili wa marehemu huo ulikutwa katika moja ya vyumba vya hotel maarufu iliopo Jijini hapa, ukiwa hauna baadhi ya viungo vya mwili kama kichwa, sehemu za siri, viganja vya mikono na matiti, huku nguo zake alizovaa pia kutoonekana.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni