Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais ( Menejimenti ya Utumishi wa Umma ), Mh Celina Kombani ( pichani ) amefariki dunia.
Katibu wa Bunge, Dk. Thomas Kashilila amesema kuwa, Waziri Kombani amefariki dunia akiwa nchini India alikokuwa anapatiwa matibabu.
" Ni kweli Waziri Kombani amefariki dunia jana jioni, na alikuwa nchini India kwa matibabu kwa karibu wiki mbili sasa, alisema Kashilila.
Waziri Kombani alikuwa mbunge wa Ulanga Mashariki kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi ( CCM ) tangu mwaka 2005, na katika uchaguzi wa mwaka huu pia alikuwa akitetea kiti hicho. Tutaendelea kuwaletea taarifa zaidi.

Hakuna maoni :
Chapisha Maoni