.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Alhamisi, 22 Oktoba 2015

LIGI YA MABINGWA BARANI ULAYA, PSG NA REAL MADRID HAKUNA MBABE, MAN CITY YAINYUKA SEVILLA NAO CSKA MOSCOW NA MAN UNITED WAGAWANA POINTI

Ligi ya mabingwa barani Ulaya imeendelea usiku wa kuamkia leo katika viwanja mbalimbali barani humo, na katika mchezo uliowakutanisha Paris St Germain ( PSG ) waliokuwa nyumbani dhidi ya wageni wao Real Madrid toka Hispania, ulishuhudia mchezo huo ukimalizika kwa timu hizo kutofungana. Katika mchezo huo timu zote zilionyesha soka la uhakika.
 MUACHE NI SHABIKI WANGU!! Mshambuliaji wa Real Madrid, Cristiano Ronaldo akimtuliza askari ( aliyevaa koti la Steward ) kutomtoa kwa nguvu uwanjani shabiki aliyekatiza kwenda kumkumbatia na kutii "kiu " yake.
Wao Manchester City wakicheza katika uwanja wao wa nyumbani usiku wa kuamkia leo wameibuka na ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya wageni wao Sevilla waliosafiri kutoka Hispania. 

Mabao kutoka kwa Adil Rami aliyejifunga katika dakika ya 3 ya mchezo huo na bao la ushindi lililwekwa kimiani na Kevin De Bruyne katika dakika ya 90 yalitosha kuwapa pointi tatu muhimu Manchester City. 

Bao la Sevilla la kufutia machozi lilifungwa na Yevhen Konoplyanka katika dakika ya 30

Katika mchezo mwingine wa ligi hiyo ya mabingwa Ulaya, Manchester United wakicheza ugenini nchini Urusi walilazimisha sare ya kufungana bao 1-1 na wenyeji wao CSKA Moscow.  

Wenyeji ndio walikuwa wa kwanza kupata bao katika dakika ya 15 likifungwa Seydou Doumbia, bao lililodumu hadi kipindi cha kwanza kinamalizika. 

Kipindi cha pili Manchester United walisawazisha bao hilo kupitia kwa Anthony Martial katika dakika ya 65.




Hakuna maoni :

Chapisha Maoni