.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumapili, 4 Oktoba 2015

LOWASSA ATINGA PEMBA, AFANYA MKUTANO MKUBWA WA KAMPENI VIWANJA VYA TIBIRINZI

WAFUASI wa vyama vinne vinavyounda UKAWA, wakimsikiliza na kumshangilia mgombea urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kwa tiketi ya CHADEMA Mhe: Edward Ngoyaye Lowassa, hayupo pichani, alipowasili kisiwani Pemba, kuzungumza na wanaukawa na kisha kuwanadi wagombea ubunge na uwakilishi wa majimbo 18 kisiwani Pemba, mkutano uliofanyika uwanja wa Tibirinzi Chake chake, (Picha na Haji Nassor, Pemba ).
MGOMBEA urais wa Zanzibar kwa tiketi ya CUF chini ya UKAWA, maalim Seif Sharif Hamad, akiwasalimia wanachama wa vyama vinavyounda UKAWA, waliohudhuria mkutano wa hadhara uliohutubiwa na Mgombea urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa tiketi ya CHADEMA, Mhe: Edward Lowassa na kufanyika uwanja wa mpira Tibirinzi Chake chake Pemba, (Picha na Haji Nassor, Pemba).
MGOMBEA Mwenza wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa tiketi ya CHADEMA Mhe: Juma Duni Haji, akizungumza na wanachama wa vyama vinavyounda UKAWA, waliohudhuria mkutano wa hadhara wa kampeni na kufanyika uwanja wa mpira Tibirinzi Chake chake Pemba, (Picha na Haji Nassor, Pemba).
MGOMBEA urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa tiketi ya CHADEMA Mhe: Edward Lowassa, akizungumza na wanachama wa vyama vinavyounda UKAWA, waliohudhuria mkutano wa hadhara wa kampeni na kufanyika uwanja wa mpira Tibirinzi Chake chake Pemba, (Picha na Haji Nassor, Pemba).
WAFUASI wa vyama vinne vinavyounda UKAWA, wakimsikiliza na kumshangilia mgombea urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kwa tiketi ya CHADEMA Mhe: Edward Ngoyaye Lowassa, hayupo pichani, alipowasili kisiwani Pemba, kuzungumza na wanaukawa na kisha kuwanadi wagombea ubunge na uwakilishi wa majimbo 18 kisiwani Pemba, mkutano uliofanyika uwanja wa Tibirinzi Chake chake, (Picha na Haji Nassor, Pemba ).
 WAANGALIZI mbali mbali wakifuatilia mkutano wa kampeni uliohutubiwa na Mgombea urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa tiketi ya CHADEMA chini ya UKAWA, Mhe: Edward Lowassa uliofanyika uwanja wa Tibirinzi Chake chake Pemba, (Picha na Haji Nassor, Pemba).
WATENDAJI wa msalaba mwekundu ‘Red cross’ wakiwatoa nje ya uwanja wa Tibirinzi Chake chake Pemba, baadhi ya wanachama wa vyama wanaounda UKAWA, baada ya kuanguka kwa joto, ambapo zaidi ya wanachama 20 walianguka uwanjani hapo, wakati wakimsikiliza mgombea urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe: Edward Lowass kwa tiketi ya CHADEMA chini ya UKAWA (Picha na Haji Nassor, Pemba).
BAADHI ya viongozi wa CHADEMA na NCCRA-MGEUZI wakifuatilia mkutano uliokuwa ukihutubiwa na mgombea urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa tiketi ya CHADEMA, chini ya UKAWA, Mhe: Edawrd Ngoyaye Lowassa, kwenye mkutano uliofanyika uwanja wa Tibirinzi Chake chake Pemba, (Picha na Haji Nassor, Pemba).
NAIBU Katibu Mkuu wa NCCR-MAGEUZI Mussa Kombo, akiwasalimia wanachama wa vyama vinavyounda UKAWA, waliohudhuria mkutano wa hadhara, uliohutubiwa na Mgombea urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa tiketi ya CHADEMA, kupitia UKAWA Mhe: Edward Lowassa na kufanyika uwanja wa mpira Tibirinzi Chake chake Pemba, (Picha na Haji Nassor, Pemba).

WAGOMBEA ubunge na uwakilishi wa majimbo 18 ya Pemba, wakinadiwa na Mgombea urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kwa tiketi ya CHADEMA chini ya UKAWA, kwenye mkutano uliofanyika uwanja wa Tibirinzi Chake chake Pemba, (Picha na Haji Nassor, Pemba).
WAGOMBEA urais Zanzibar na Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, na mgombea mwenza Juma Duni Haji (kulia), wakijadili jambo kabla ya kuondoka kwenye uwanja wa Tibirinzi Chake chake, ambapo kulifanyika mkutano wa hadhara uliohutubiwa na Mgombea urais wa Muungano wa tiketi ya CHADEM Mhe: Edward Lowassa, (Picha na Haji Nassor, Pemba).

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni