.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Ijumaa, 20 Novemba 2015

NAIBU KAMISHNA MKUU WA SHIRIKA LA UMOJA WA MATAIFA LA KUHUDUMIA WAKIMBIZI (UNHCR) NA UJUMBE WAKE WATEMBELEA WIZARA YA MAMBO YA NDANI YA NCHI

NI1
Uongozi wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi ukiwa katika kikao na Ujumbe wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Wakimbizi (UNHCR) uliotembelea Wizara hiyo. Wa pili kulia ni Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, John Mngodo.
NI2
Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, John Mngodo akizungumza na ujumbe wa Shrika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Wakimbizi (UNHCR) (haupo pichani) uliotembelea Wizara hiyo ambapo masuala mbalimbali kuhusiana na wakimbizi yalijadiliwa. Tanzania ni mojawapo ya nchi zinazohifadhi wakimbizi, hasa kutoka Ukanda wa Maziwa Makuu.
NI3
Naibu Kamishna Mkuu wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Wakimbizi (UNHCR), Bi. Kelly Clements akizungumza katika kikao na Uongozi wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi (haupo pichani) wakati yeye na ujumbe wake walipotembelea Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi. Katikati ni Mkurugenzi wa UNHCR, Kanda ya Afrika na kushoto ni Mtendaji Msaidizi wa Naibu Kamishna Mkuu wa UNHCR, Bi. Geraldine Salducci.
NI4
Mkurugenzi wa Idara ya Wakimbizi katika Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Harrison Mseke akizungumza katika kikao cha Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi na ujumbe wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Wakimbizi (UNHCR) wakati ujumbe huo ulipotembelea Wizara. Kulia ni Naibu Katibu Mkuu wa Wizara hiyo.

(Picha zote na Abubakari Akida,Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi)

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni