.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumanne, 3 Novemba 2015

TWIGA KUMUAGA CHABURUMA JUMAMOSI

Mshambuliaji wa timu ya Taifa ya Wanawake ya Tanzania ‘Twiga Stars’ Estha Chaburuma ‘Lunyamila’ ataagwa rasmi katika mchezo wa kirafiki kati ya timu ya Taifa ya Tanzania ya Wanawake ‘Twiga Stars’ dhidi ya timu ya taifa ya wanawake ya Malawi utakaochezwa siku ya jumamosi katika uwanja wa Azam Complex Chamazi jijini Dar es salaam.

Chaburuma amekua ni miongoni mwa wachezaji waanzilishi wa Twiga Stars ambapo amekua akiitumikia timu hiyo tangu kuanzishwa kwake mpaka sasa timu inapojiandaa na mchezo dhidi ya Malawi.

Mwenyekiti wa Kamati ya Soka la Wanawake ya TFF, Amina Karuma amesema wameamua kutumia mchezo huo wa kirafiki kwa ajili ya kumuaga Chabruma ambaye amekua ni chachu ya maendeleo ya mpira wa miguu kwa wanawake, kutokana na kuwafanya wanawake wengi kujitokeza kucheza mchezo huo.

Naye kocha wa timu hiyo, Rogasian Kaijage amesema vijana wake wapo katika hali nzuri, wananadelea na maandalizi ya mchezo huo wa jumamosi, ambapo anaimani watautumia vizuri katika kumuaga mchezaji mwenzao wa siku nyingi.


Hakuna maoni :

Chapisha Maoni