.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumatatu, 28 Desemba 2015

RAIS ATAKA WALIOANDA TAMASHA LA ENRIQUES IGLESIAS WACHAPWE BAKORA

Rais wa Sri Lanka amesema kuwa waandaaji wa tamasha la Enrique Iglesias, wanapaswa kupigwa bakora kutokana na tabia isiyofaa iliyoonyeshwa na baadhi ya mashabiki wanawake katika tamasha hilo.

Rais Maithripala Sirisena amesema picha za baadhi ya wanawake walioonekana wakimkimbilia Iglesias na kumbusu pamoja na kumrushia nguo zao za ndani si za kistaarabu hata kidogo.

Rais Sirisena amesema waandaaji wa tamasha la Enrique Iglesias wanapaswa kuchapwa na mijeledi wenye vitu vya kuchoma, akimaanisha adhabu kali iliyokuwa ikitoolewa katika mika ya kale.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni