.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Alhamisi, 14 Januari 2016

JKT MLALE YAFUZU HATUA YA 16 BORA


Michezo ya Kombe la Shirikisho (Azam Sports Federation Cup) mzunguko wa tatu imeendelea kwa mchezo mmoja kuchezwa mjini Songea, ambapo timu ya JKT Mlale imeiondosha Majimaji kwa mabao 2-1.

Michuano hiyo ambayo Bingwa wake ataiwakilisha Tanzania kwenye kombe la Shirikisho Afrika 2017 (CC), imekua ya kuvutia na hasa kwa timu za madaraja ya chini kuziondosha timu za mdaraja ya juu.

JKT Mlale imekua timu ya kwanza kutoka daraja la kwanza kufuzu kwa hatua ya 16 bora, ambapo sasa inasubiria washindi wengine 15 kutoka katika michezo itakayochezwa wikiendi ya Januari 23-17, 2015.

Mpaka sasa kuna timu za saba za daraja la Pili zinawania kufuzu kwa hatua ya nne, timu hizo ni Abajalo (Dasm), Madini (Arusha), Mvunvuma (Kigoma),

Pamba (Mwanza), Wenda (Mbeya), Mshikamano (Dsm), na Singida United (Singida), huku za daraja la kwanza timu 8 zikisaka nafasi ya kuingia hatua ya 16.

Timu za daraja la kwanza ni Ashanti United (Dsm), Burkinafaso (Morogoro), Friends Rangers (Dsm), Geita Gold (Geita), Lipuli (Iringa), Njombe (Njombe), Panone (Kilimanjaro) na Rhino Rangers (Tabora).

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni