.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumanne, 19 Januari 2016

MISA YA KUMBUKUMBU YA MAREHEMU LETICIA NYERERE

Misa ya kumbukumbu ya marehemu Leticia Nyerere iliyofanyika siku ya Jumamosi January 16, 2016 katika kanisa la Mt. Edward Baltimore, Maryland na kuhudhuriwa na ndugu, jamaa na marafiki kutoka kila kona ya Marekani. Mwili wa marehemu Leticia Nyerere unatarajia kufika Tanzania kesho Jumanne January 19, 2016 na utaagwa Dar es Salaam na mazishi yake yanatarajiwa kufanyika Butiama. Picha na Iska Jojo.
Wana familia wakifuatilia misa ya kumbukumbu ya marehemu Leticia Nyerere iliyofanyika siku ya Jumamosi January 16, 2016 katika kanisa la Mt. Edward Baltimore, Maryland nchini Marekani. Kutoka kushoto ni Bi. Kijogoo kutoka Arizona,,Margareth Mageni na ,Flora Mageni
Wanafamilia wakiwemo watoto wa marehemu kutoka kushoto ni Julius Nyerere, Helena Nyerere na Julia Nyerere kulia ni Edlaila Nyerere ambaye ni wifi wa marehemu kutoka Atlanta jimbo la Georgia nchini Marekani wakifuatilia misa ya kumbukumbu ya mpendwa mama yao Leticia Nyerere aliyeaga Dunia siku ya Jumapili January 10, 2016 katika hospitali ya Jumuiya ya Madaktari iliyopo Lanham, maryland nchini Marekani.
Balozi wa Tanzania nchini Marekani Mhe. Wilson Masilingi akitoa mkono wa pole kwa mume wa marehemu Madaraka Nyerere kwenye misa ya kumbukumbu ya marehemu Leticia Nyerere iliyofanyika siku ya Jumamosi January 16, 2016 katika kanisa la Mt. Edward Baltimore, Maryland na kuhudhuriwa na ndugu, jamaa na marafiki
             Balozi Wilson Masilingi akiongea machache na kutoa pole kwa wafiwa.
Bi Resty Budodi Semali rafiki wa marehemu kutoka Atlanta akiongea jambo ya jinsi alivyomfahamu marehemu.
                                                         Bhoke Nyerere kutoka Canada akisoma neno.
           daktari wa familia Dr. Ndubisi akiongea jinsi alivyomfahamu marehemu.
    Katibu mwenezi wa CCM DMV akielezea jinsi gani alivyomfahamu marehemu
Rais wa Jumuiya ya Watanzania DMV akitoa salamu za rambirambi kwa wafiwa na kuelezea jinsi gani alivyomfahamu marehemu.
Pius Mtalemwa mmoja wa viongozi wa Jumuiya ya Wakatoliki DMV akisema machache ya jinsi alivyomfahamu marehemu.
                        Watoto wa marehemu kutoka kushoto ni Julia, Julius na Helena.
BOFYA HAPA KWA PICHA ZAIDI


Hakuna maoni :

Chapisha Maoni