.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Ijumaa, 29 Januari 2016

MWILI WA SWAI KUSAFIRISHWA LEO


Shirikisho la Mpira wa Miguu nchini (TFF) linapenda kuwajulisha wapenzi, wadau, wa mpira wa miguu nchini kuwa, mwili wa aliyekua Mjumbe wa Kamati ya Utendaji ya TFF na Mwenyekiti wa Chama cha Mpira wa Miguu mkoa wa Simiyu, Epaphra Swai utaangwa leo saa 9 alasiri katika hosiptali ya Muhimbili, na baadae saa 11 jioni itaanza safari ya kuelekea mkoani Kilimanjaro.

Ibada ya kuuaga mwili wa marehemu itafanyika leo Ijumaa saa 9 alasiri katika hospitali ya Muhimbili, ambapo ndugu, jamaaa, marafiki na wadau wa mpira wa miguu nwatapana nafasi ya kutoa heshima zao za mwisho kwa mwili wa marehemu Epaphra Swai, na baadae majira ya saa 11 jioni itaanza safari ya kuelekea Machame mkoani Kilimanjaro.

Mazishi ya marehemu Epaphra Swai yatafanyika kesho Jumamosi mchana nyumbani kwako Machame Kilimanjaro.

Shirikisho la Mpira wa Miguu nchini (TFF) inatoa pole kwa ndugu, jamaa, marafiki, wadau wa mpira wa miguu pamoja na familia ya marehemu, na kusema wako pamoja nao katika kipindi hiki kigumu cha maombelezo ya msiba huo.

Marehemu Epaphra Swai alifariki dunia jana asubuhi katika hospital ya taifa ya Muhimbili.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni