Neymar amepachika goli wakati
Barcelona ikishinda kwa mabao 2-1 katika mchezo wa robo fainali wa
kwanza ya kombe la Copa del Rey dhidi ya Athletic Bilbao kwenye dimba
la San Mames.
Mabigwa hao watetezi wa kombe hilo
walicheza bila Lionel Messi aliyepumzishwa pamoja na Luis Suarez
anayetumikia adhabu, lakini walipata mabao 2 ndani ya dakika 25 za
mwanzo.
Barcelona ilipata goli la kwanza
kupitia kwa Munir el Haddadi aliyeunganisha wavuni krosi ya Ivan
Rakitic, kabla ya Neymar kufunga bao la pili.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni