.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumamosi, 16 Januari 2016

SERGIO AGUERO AIPAISHA MAN CITY HUKU CHELSEA IKIBANWA

Manchester City imekwea kileleni mwa Ligi Kuu ya Uingereza kwa muda baada ya kuichakaza Crystal Palace kwa mabao 4-0, kabla ya Leicester kurejea tena kileleni baadae.

Katika mchezo huo mshambuliaji Sergio Aguero alipachika mabao mawili katika mchezo huo, ambao ulishuhudia pia David Silva akitikisa nyavu, huku bao la kwanza likipachikwa na Fabian Delph.
Sergio Aguero akiachia shuti lililoingia wavuni na kuandika bao lake la pili katika mchezo huo
Katika mechi nyingine John Terry amefunga bao lililozua utata katika dakika ya 98, na kuipatia Chelsea pointi moja baada ya kutoka sare ya mabao 3-3 dhidi ya Everton.

Everton walianza kuongoza baada ya Terry kujifunga, na kisha Kevin Mirallas kufunga bao la pili, hata hivyo Diego Costa na Cec Fabregas walisawazisha na kufanya matokeo kuwa 2-2.

Ramiro Funes Mori aliongeza bao la tatu kwa Everton katika dakika ya 90, kabla ya John Terry kusawazisha kwa bao la kisigino ambalo inasadikiwa kuwa alikuwa ameotea kabla ya kufunga.
                         John Terry akifurahia goli alilofunga na mashabiki wa Chelsea

Katika mechi zingine za Ligi Kuu ya Uingereza matokeo yalikuwa Tottenham 4 - 1Sunderland, Bournemouth 3- 0 Norwich, Man City 4 – 0 Crystal Palace, Newcastle 2 - 1West Ham, Southampton 3- 0 West Brom na Aston Villa1- 1 Leicester.


Hakuna maoni :

Chapisha Maoni