.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumamosi, 30 Januari 2016

SWAI KUZIKWA LEO KNCU - SAWE


Aliyekua Mjumbe wa Kamati ya Utendaji ya TFF, na Mwenyekiti wa Chama cha Mpira wa Miguu mkoa wa Simiyu, Epaphra Swai anatarajiwa kuzikwa leo jioni saa 10 katika kijiji cha Sawe, Masama Mashariki.

Ibada ya kuuaga mwili wa marehemu itafanyika leo Jumamosi saa 9 alasiri, kitongoji cha Ituuny kijiji cha Sawe, na mazishi yake yatafanyika katika eneo la KNCU kata ya Masama Mashariki.

Shirikisho la Mpira wa Miguu nchini (TFF) linaendelea kutoa pole kwa ndugu, jamaa, marafiki, wadau wa mpira wa miguu pamoja na familia ya marehemu, katika kipindi hiki kigumu cha maombelezo ya msiba huo.

Marehemu Epaphra Swai aliaga dunia Alhamisi asubuhi katika hospital ya taifa ya Muhimbili.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni