.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumanne, 19 Januari 2016

VPL MZUNGKO WA 15 KUENDELEA KESHO


Ligi Kuu ya Vodacom mzunguko wa 15 unatarajiwa kuendelea kesho Jumatano kwa michezo mitano, na Alhamisi kwa michezo mitatu kwa kila timu kusaka pointi tatu muhimu katika mzunguko huo.

Uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam, Maafande wa JKT Ruvu watawakaribisha Simba SC, Ndanda FC watakua wenyeji wa Mbeya City kwenye uwanja wa Nangwanda Sijaona.

Tanzania Prisons watakua wenyeji wa Coastal Union katika uwanja wa Sokoine jijini Mbeya, Stand United watacheza dhidi ya Toto Africans kwenye uwanja wa Kambarage, huku Mgambo Shooting wakiwakaribisha Azam FC kwenye uwanja wa Mkwakwani jijini Tanga.

Alhamisi ligi hiyo itaendelea kwa michezo mitatu, Mwadui FC watawakaribisha Kagera Sugar katika uwanja wa Mwadui, African Sports watakua wenyeji wa Mtibwa Sugar uwanja wa Mkwakwani jijini Tnaga, huku Young Africans wakiwakaribisha Majimaji FC katika uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni