Beki wa Chelsea Kurt Zouma atakuwa
nje ya uwanja kwa miezi sita kutokana na kuhitaji kufanyiwa upasuaji
kwenye goti baada ya kupata jeraha jumapili.
Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka
21, alianguka vibaya baada ya kuwania mpira wa juu alitolewa akiwa
amebebwa kwenye machela katika mchezo wao na Manchester United.
Vipimo vya scan vilivyofanywa leo
vimeonyesha kuumia kwa mishipa ya ligament, ambapo atafanyiwa
upasuaji wiki hii.


Hakuna maoni :
Chapisha Maoni