Kocha wa Manchester United, Louis
van Gaal amesema kichapo alichopata cha mabao 2-1 kutoka kwa FC
Midtjylland kinaendana na sheria ya Murphy, ambayo inasema kitu
kisicho fanya vyema hakitofanya vyema.
Katika mchezo huo Memphis Depay
aliipatia goli la kwanza Manchester United wakiwa ugenini katika
mchezo wao wa awali wa Ligi ya Uropa hatua ya 32 bora, lakini Pione
Sisto na Paul Onuachu waliwapatia wenyeji ushindi.
Kocha Van Gaal, ambaye kwa sasa hana
wachezaji 13 kutokana na kuwa majeruhi, amempoteza pia kipa David de
Gea wakati wa mazoezi ya kupasha joto mwili, hii sasa inamaanisha
kitu kisicho fanya vyema hakitofanya vyema.
Kipa Sergio Romero akipangua kimiujiza kwa mkono mmoja mpira wa kichwa na kuokoa goli


Hakuna maoni :
Chapisha Maoni