Timu ya Liverpool imepangiwa na
mahasimu wao wa Uingereza Manchester United katika michuano ya Uropa
hatua ya 16 bora.
Timu hizo zote zikiwa hazipo katika
nafasi ya nne ya bora katika Ligi Kuu ya Uingereza, zitawania
kushinda taji hilo, ili zipate fursa ya kutinga Ligi ya Mabingwa
Ulaya mwakani.
Timu hizo mbili zitakutana mara
mbili ndani ya siku saba, mechi ya kwanza ikiwa katika dimba la
Anfield Machi 10 na wa marudio Old Trafford on Machi 17.
Droo nyingine ni Shakhtar Donetsk v
Anderlecht, Basel v Sevilla, Villarreal v Bayer Leverkusen, Athletic
Bilbao v Valencia, Sparta Prague v Lazio, Borussia Dortmund v
Tottenham na Fenerbahce v Braga

Hakuna maoni :
Chapisha Maoni