.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Alhamisi, 11 Februari 2016

MALINZI AMPONGEZA MWENDWA WA FKF


Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Jamal Malinzi ametuma salamu za pongezi kwa Rais mpya wa Shirikisho la Mpira wa Miguu nchini Kenya (FKF), Nick Mwendwa kwa kuchaguliwa kuliongoza shirikisho hilo.

Katika salamu hizo, Malinzi amempongeza Mwendwa kwa nafasi hiyo aliyopewa kuliongoza soka la nchini Kenya, na kuahidi TFF itaendelea kushirikiana nae katika maendeleo ya mpira wa miguu kwa ukanda huu wa Afrika Mashariki.

Nick Mwendwa alishinda nafasi hiyo jana katika uchaguzi uliofanyika jijini Nairobi kwa kupata alama 50 kati ya 77 za wapiga kura wote na kupata nafasi hiyo iliyokua inashikiliwa na Samwel Nyamweya aliyemaliza muda wake.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni