.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumatano, 9 Machi 2016

BALOZI SEIF AWEKA JIWE LA MSINGI KATIKA SKULI YA KWARARA NA KITUO CHA HABARI NA MAWASILIANO CHA TUMAINI

Mandhari ya eneo linalojengwa Skuli ya Ghorofa kwarara pamoja na Kituo cha Habari na Mawasliniano cha Tumaini Wilaya ya Magharibi “B” unaofadhiliwa kwa pamoja kati ya mashirikia matatu ya Good Neighbors, Shirika la Habari la Korea Kusini {SBS } pamoja na Shirika la Maendeleo ya Korea Kusini KOICA.
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi akiweka jiwe la msingi la Ujenzi wa Skuli ya Ghorofa na Kituo cha Habari na Mawasiliano cha Tumaini hapo Kwarara Wilaya ya Magharibi.
Msimamizi wa Ujenzi wa Skuli mpya ya Ghorofa ya Kwarara Mhandisi Ali Mrabouk akimfahamisha Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif ramani ya ujenzi wa majengo ya Skuli ya Ghorofa ya Kwarara pamoja na Kituo cha Habari na Mawasiliano cha Tumaini.
Balozi wa Korea ya Kusini Nchini Tanzania Bwana Songo akitoa salamu kwenye hafla ya uwekaji wa jiwe la Msingi la Skuli ya Ghorofa pamoja na Kituo cha Habari na Mawasiliano zinazojengwa kwa msaada wa mashirika ya Nchi hiyo.
Wanafunzi wa skuli za msingi wanaosoma kwenye shehia ya Kwarara wakishangiria matukio mbali mbali kwenye hafla ya uwekaji wa jiwe la msingi la skuli ya ghorofa ya eneo hilo.(Picha na – OMPR – ZNZ.)

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni