Kampuni ya Nike imesitisha udhamini
kwa Maria Sharapova saa kadhaa baada ya kukiri kutumia dawa za
kututumua misuli zilizopigwa marufuku katika michuano ya wazi ya
Australia mwezi januari.
Mshindi huyo wa Grand Slam mara tano
amebainisha kutenda kosa hilo katika mkutano wake na waandishi wa
habari katika hoteli Jijini Los Angeles, akikiri kuwa amenaswa na
chombo cha kupinga matumizi ya dawa hizo katika mchezo wa tenesi.
Mchezaji tenesi huyo anayelipwa mno
kuliko wachezaji mwingine yoyote mwanamke katika mchezo huo,
amebainika kutumia dawa aina ya Mildronate ama Meldonium, ambayo
ilipigwa marufuku Januari mosi mwaka huu.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni