Timu ya Barcelona imeibuka kwa kasi
kutoka usingizini baada ya kuchezea vichapo katika mechi tatu za
nyuma za La Liga na kuichakaza Deportivo La Coruna kwa magoli 8-0.
Katika mchezo huo Luis Suarez
alifunga magoli manne, Rakitic kuongeza la tano, Messi akafunga la
sita, Bartra akatumbukiza la saba kabla ya Neymar hajakamilisha la
nane.
Luis Suarez akifunga goli la kwanza
Neymar akimchambua kipa wa deportivo la Coruna na kupachika goli
Nayo Real Real Madrid imeendelea
kuzifukuzia kileleni Barcelona na Atletico Madrid latika Ligi Kuu ya
Hispania ya La Liga kwa ushindi wa mabao 3-0 dhidi ya Villarreal
kwenye dimba la Bernabeu.
Goli la kichwa la Karim Benzema
liliifanya Real Madrid iongoze katika kipindi cha kwanza, na katika
kipindi cha pili Lucas Vazquez akafunga la pili kabla ya Luka Modric
kuhitimisha la tatu, na kuipa Real Madrid ushindi wa nane mfululizo.
Benzema akipachika goli kwa mpira wa kichwa





Hakuna maoni :
Chapisha Maoni