.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumanne, 12 Aprili 2016

WAZIRI MAHIGA APOKEA NAKALA ZA HATI ZA UTAMBULISHO KUTOKA KWA MABALOZI WATEULE WA SUDAN KUSINI NA JAMUHURI YA CZECH

Waziri wa Mambo ya Nje Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Kikanda na Kimataifa Balozi Augustine Mahiga (kulia) akipokea Nakala za Hati za Utambulisho kutoka kwa Balozi mteule wa Jamhuri ya Czech, Mhe. Pavel Rezac, na kisha kufanya nae mazungumzo yaliyojikita katika kukuza ushirikiano kati ya Tanzania na Jamhuri ya Czech.
                        Waziri Mahiga akizungumza na Balozi Mteule Mhe. Pavel Rezac
Waziri Mahiga akiwa katika picha ya pamoja na Balozi Mteule wa Jamhuri ya Czech Mhe. Pavel Rezac.
Waziri wa Mambo ya Nje Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Kikanda na Kimataifa Balozi Augustine Mahiga (kulia) akipokea Nakala za Hati za Utambulisho kutoka kwa Balozi mteule wa Jamhuri ya Sudani Kusini, Mhe. Mariano Deng Ngor, na kisha kufanya nae mazungumzo yaliyojikita katika kukuza Ushirikiano katika sekta mbalimbali kati ya Tanzania na Jamhuri ya Sudani Kusini.
        Waziri Mahiga akizungumza na Balozi Mteule Mhe. Mariano Deng Ngor
Waziri Mahiga (wa pili kutoka kulia) akiwa katika picha ya pamoja na Balozi Mteule wa Jamhuri ya Sudani Kusini Mhe. Mariano Deng Ngor (wa tatu kutoka kushoto), Mkurugenzi wa Idara ya Afrika Balozi Samwel Shelukindo (wa kwanza kushoto), Afisa Ubalozi wa Sudani Kusini nchini (wa pili kutoka kulia) na Afisa Mambo ya Nje, Bw. Eric Ngilangwa (wa kwanza kulia).

                                                                                                Picha na Reginald Philip.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni