.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Alhamisi, 5 Mei 2016

KAMPUNI YA ZTE WAMKABIDHI MAMA MWANAMWEMA MSAADA WAO KWA AJILI YA KAMBI YA KIPINDUPINDU

Mke wa Rais wa Zanzibar Mama Mwanamwema Shein, akisalimiana na Mke wa Balozi Mdogo wa Chini Zanzibar Bi Wu Yan.
Mke wa Rais wa Zanzibar Mama Mwanamwema Shein, akisalimiana na Meneja Mkaazi wa Kampuni ya ZTE Afrika Mashariki,Zhu Yu, alipofika Ikulu Migombani kukabidhi msaada kwa ajili ya Wananchi waliopata Maafa ya Mvua za Masika Zanzibar.
 Meneja Mkaazi wa Kampuni ya ZTE Afrika Mashariki,Zhu Yu, akizugumza wakati wa hafla hiyo ya kukabidhi misaada yao kwa Mke wa Rais wa Zanzibar Mama Mwanamwema Shein Ikulu Migombani Zanzibar. akiwa na ujumbe wake.
Mke wa Rais wa Zanzibar akizungumza na Ujumbe wa Kampuni ya ZTE ukiwa na Mke wa Balozi Mdogo wa Chini Bi Wu Yan, uliofika Ikulu Migombani Zanzibar kuonana na Mama Mwanamwema na kumkabidhi msaada wao kwa Wananchi waliopata maafa ya Mvua za Masika na wa Kambi ya Kipindupindu
Mke wa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mama Mwanamwema Shein, akipokea msaada wa madaftari na vifaa vingine kutoka kwa Meneja Mkaazi wa Kampuni ya ZTE Afrika Mashariki,Zhu Yu,kwa ajili ya Watoto na Wananchi waliopata Maafa ya Mvua za Masika zilizonyesha hivi karibuni, hafla hiyo ya makabidhiano imefanyika katika ukumbi wa Ikulu Migombani Zanzibar.
Mke wa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mama Mwanamwema Shein, akipokea msaada wa mashuka na vifaa vingine kutoka kwa Meneja Mkaazi wa Kampuni ya ZTE Afrika Mashariki,Zhu Yu,kwa ajili ya Wananchi waliopata Maafa ya Mvua za Masika zilizonyesha hivi karibuni, hafla hiyo ya makabidhiano imefanyika katika ukumbi wa Ikulu Migombani Zanzibar..
Mke wa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mama Mwanamwema Shein, akipokea msaada wa sabuni za maji na vifaa vingine kutoka kwa Meneja Mkaazi wa Kampuni ya ZTE Afrika Mashariki,Zhu Yu,kwa ajili ya Wananchi waliopata Maafa ya Mvua za Masika zilizonyesha hivi karibuni, hafla hiyo ya makabidhiano imefanyika katika ukumbi wa Ikulu Migombani Zanzibar.
Mke wa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mama Mwanamwema Shein, akiwa katika picha ya pamoja na Mke wa Balozi Mdogo wa China Zanzibar na Ujumbe wa Kampuni ya ZTE.
Meneja Mkaazi wa Kampuni ya ZTE Afrika Mashariki,Zhu Yu, akiagana na Mke wa Rais wa Zanzibar Mama Mwanamwema Shein, baada ya kumaliza hafla ya kukabidhi msaada.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni