.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumatatu, 16 Mei 2016

KINDA MARCUS RASHFORD AITWA KIKOSI CHA UINGEREZA

Mshambuliaji kinda wa Manchester United, Marcus Rashford, 18, amezidi kupanda baada ya kuingizwa katika kikosi cha wacheaji 26 wa Uingereza kitakachoshiriki michuano ya Ubingwa wa Ulaya.

Kinda huyo aliyeanza kuchezea timu ya wakubwa ya Manchester United Februari mwaka huu, amechaguliwa na kocha Roy Hodgson hii leo katika kikosi kinachojiandaa na michezo ya maandalizi dhidi ya Uturuki, Australia na Ureno, kabla ya michuano hiyo Ufaransa.

Katika kikosi hicho cha Uingereza pia yumo winga Andros Townsend aliyeitwa na kocha Hodgson baada ya kumaliza vyema Ligi Kuu ya Uingereza akiwa na timu yake iliyoshuka daraja ya Newcastle. 
                                         Kocha wa timu ya taifa ya Uingereza Roy Hodgson

 Kikosi Kizima Cha Uingereza ni Kama ifuatavyo:-

Makipa: Fraser Forster (Southampton), Joe Hart (Manchester City), Tom Heaton (Burnley)

Mabeki: Ryan Bertrand (Southampton), Gary Cahill (Chelsea), Nathaniel Clyne (Liverpool), Danny Rose (Tottenham), Chris Smalling (Manchester United), John Stones (Everton), Kyle Walker (Tottenham)

Viungo: Dele Alli (Tottenham), Ross Barkley (Everton), Fabian Delph (Manchester City), Eric Dier (Tottenham), Danny Drinkwater (Leicester City), Jordan Henderson (Liverpool), Adam Lallana (Liverpool), James Milner (Liverpool), Raheem Sterling (Manchester City), Andros Townsend (Newcastle), Jack Wilshere (Arsenal)

Washambuliaji: Harry Kane (Tottenham), Marcus Rashford (Manchester United), Wayne Rooney (Manchester United), Daniel Sturridge (Liverpool), Jamie Vardy (Leicester City).

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni