Dogo Marcus Rashford ametakata
wakati Manchester United ikitwaa nafasi ya kutinga hatua ya makundi
ya Ligi ya Uropa kufuatia kuifunga Bournemouth mabao 3-1 katika mchezo wa Ligi Kuu ya Uingereza usiku wa kuamkia leo.
Mchezo huo wa jana ulishuhudiwa na
mashabiki wachache katika dimba la Old Trafford, baada ya jumapili
kuhairishwa kutokana na tishio la bomu ambapo baadaye ilibainika kuwa
ni bomu feki.
Mkongwe Wayne Rooney alikuwa wa
kwanza kuipatia Manchester United goli la kwanza, huku dogo anayekuja
juu Marcus Rashford akifunga goli la pili kabla ya Ashley Young
kupachika goli la tatu. Bournemouth walipata goli pekee baada ya
Chris Smalling kujifunga.
Ashley Young akiachia shuti lililojaa wavuni na kuandia goli la tatu
Mashabiki wa Man U wakishinikiza kwa njia ya bango kocha Louis van Gaal aondoke
Asanteni kwa Kuja: Kocha Louis van Gaal akiwashukuru mashabiki




Hakuna maoni :
Chapisha Maoni