.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Alhamisi, 19 Mei 2016

MASHABIKI WA SEVILLA NA LIVERPOOL WATWANGANA WAKATI WA FAINALI YA EUROPA LIGI

Mchezo wa fainali wa ligi ya Europa uliozikutanisha timu za Sevilla toka Hispania na Liverpool toka Uingereza na kumalizika kwa Sevilla kulitwaa kombe hilo kwa mara ya tatu mfululizo, ulishuhudia vurugu toka kwa mashabiki wa timu zote mbili. Mchezo huo uliofanyika Basle katika uwanja wa St Jakob-Park, ulimalizika kwa Liverpool kuchapwa 3-1
Vurugu hizo zilitokea katika moja ya jukwaa ambalo lilitumiwa na mashabiki wa timu zote mbili ambapo ngumi na mateke zilitawala huku mashabiki wa Sevilla wakionekana kuwa chanzo na wenye fujo zaidi.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni