Maziko ya mmoja wa wanamuziki
wakubwa barani Afrika, Papa Wemba, yanafanyika leo Jijini Kinshasa
katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo.
Umati mkubwa umekusanyika nje ya
Kanisa la Notre Dame, ambako ibada ya watu wa karibu na familia
inafanyika. Kabla ya kuzikwa baadaye Jijini Kinshasa.
Wemba, 66, aliyepachikwa jina la
Mfalme rumba, alifariki baada ya kuanguka jukwaani nchini Ivory
Coast Aprili 24.
Ibada ya kuuombea mwili wa Papa Wemba ikiendelea kanisani
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni