Timu ya Liverpool imejikuta
ikipoteza mchezo katika kipindi cha pili na kuiwezesha Sevilla kutwaa
Kombe la Ligi ya Uropo kwa mara ya tatu mfululizo katika mchezo
uliochezwa jana usiku.
Kikosi cha kocha Jurgen Klopp
kilionekana kama kimejipanga kutwaa kombe hilo katika mchezo huo wa
fainali wakati Daniel Sturridge alipofanya shambulizi nzuri na
kuipatia Liverpool goli la kuongoza.
Kazi hiyo nzuri ya ya Sturridge
ilikuja kutibuka katika sekunde 17 za mwanzoni mwa kipindi cha pili
baada ya Kevin Gameiro kuutumbukiza wavuni mpira wa krosi iliyopigwa
na Mariano Ferreira na kuisawazishia Sevilla. Sevilla iliongeza
magoli mengine mawili kupitia Andújar Moreno Coke.
Daniel Sturridge akipiga mpira kwa guu la kushoto na kujaa wavuni
Muuaji wa Liverpool Andújar Moreno Coke akipachika goli lake la pili
Daniel Sturridge akiwa amekaa chini uwanjani asiamini kilichotokea




Hakuna maoni :
Chapisha Maoni