Shabiki wa Manchester United
aliyejibana fedha zake na kusafiri kutoka Sierra Leone kuja kuiona
klabu yake ikicheza mchezo wa mwisho wa Ligi Kuu ya Uingereza
alijikuta katika wakati mgumu baada ya mchezo huo kuhairishwa kwa
tishio la bomu feki.
Moses alikuwa ni miongoni mwa
mashabiki wa Manchester United waliojikuta wakichanganyikiwa jana
baada ya tukio hilo, lakini alipata faraja baada ya mashabiki wenye
moyo wa huruma kumlipia tiketi ya ndege na kuingia uwanjani kuja
kuiona Manchester United katika mchezo wa fainali ya Kombe la FA.
Moses akiwa amechanganyikiwa huku mishipa ya kichwani ikimtoka baada ya mchezo wa Manchester United kuhairishwa hapo jana.


Hakuna maoni :
Chapisha Maoni