Kocha Jurgen Klopp anaonekana
kuelekea kutwaa kikombe chake cha kwanza katika msimu huu akiwa na
Liverpool baada ya kuishinda Villarreal na kutinga fainali ya Ligi ya
Uropa.
Ikiwa imefungwa goli moja katika
mchezo wa awali, Liverpool ilisawazisha kupitia goli la mapema la
kujifunga la Bruno Soriano.
Daniel Sturridge, aliyeachwa katika
mchezo wa Hispania, aliipatia Liverpool goli la pili Liverpool kwa
mpira wa chini, ikiwa ni kazi nzuri iliyofanywa na Roberto Firmino na
Adam Lallana akaongeza la tatu.
Daniel Sturridge akipachika goli la pili la Liverpool
Adam Lallan akifunga goli la tatu katika mchezo huo
Timu ya Sevilla inaendelea vyema
katika jitihada zake za kutwaa kwa mara ya tatu mfululizo ubingwa wa
Ligi ya Uropa baada ya kuifunga Shakhtar Donetsk na sasa itakutana na
Liverpool kwenye fainali.
Baada ya kutoka sare ya mabao 2-2
katika mchezo wa kwanza uliopigwa nchini Ukraine, Sevilla ilianza
vyema mchezo huo wa pili kwa kufunga goli kupitia kwa Kevin Gameiro,
kabla ya mchezaji wa zamani wa Arsenal Eduardo kusawazisha.
Gameiro tena aliipatia Sevilla goli
la pili baadae Mariano Ferreira kuongeza la tatu na kufanya matokeo
kuwa Sevilla 3-1 Shakhtar Donetsk.
Mariano Ferreira akifurahi goli la tatu la Sevilla alilofunga
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni