Mabasi mengi ya abiria nchini Kenya
maarufu kama Matatu katika Jiji la Nairobi yana kunguni hali ambayo
inatatiza biashara ya usafiri katika Jiji hilo Kuu la Kenya.
Wadudu hao wanaonyonya damu sasa
wanatishia kuathiri biashara ya usafirishaji abiria Jijini Nairobi,
kutokana na watu wengi kuhofia huduma za mabasi hayo.
Kunguni hao wamekuwa wakilitwa
kwenyea mabasi na abiria bila ya kufahamu kutokea nyumbani kwaona
kuishia kwenye viti.
Kwa sasa watoaji usafiri huo wa umma
wameanza kampeni ya kukabiliana na kunguni kwa kunyunyuzia dawa na
kuwataka abiria kuwasilisha malalamiko yao iwapo wataona kunguni
kwenye Matatu.
Wadudu kunguni waliovamia mabasi ya Matatu Jijini Nairobi
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni