Nchi
ya Poland imetinga hatua ya robo fainali ya michuano ya Euro 1016 kwa
mara ya kwanza katika historia ya nchi hiyo, baada ya Grzegorz
Krychowiak kufunga penati muhimu, katika ushindi uliopatikana kwa
mikwaju ya penati 5-4 dhidi ya Switzerland.
Katika
mchezo huyo mchezaji mpya wa Arsenal Granit Xhaka alijikuta
akivunjika moyo baada ya kuwa mchezaji pekee aliyekosa penati katika
mchezo huo huko Saint-Etienne, kwa kupiga mpira nje ya goli.
Mchezo
huo uliingia katika hatua ya mikwaju ya penati baada ya mchezaji wa
timu ya Stoke City Xherdan Shaqiri kufunga goli bora kwa sasa katika
michuano hiyo kwa kuupiga mpira kwa tiki taka na kufanya matokeo yawe
1-1.
Granit Xhaka akipiga nje ya goli mkwaju wa penati
Xherdan Shaqiri akipiga mpira kwa staili ya tiki taka na kusawazisha goli
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni