.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumamosi, 18 Juni 2016

ROMELU LUKAKU AISAIDIA UBELGIJI KUPATA USHINDI WAKE WA KWANZA EURO 2016

Mshambuliaji Romelu Lukaku amefumania nyavu mara mbili wakati Ubelgiji ikipata ushindi wake wa kwanza katika michuano ya Euro 2016 na kuichakaza Jamhuri ya Ireland kwa magoli 3-0.

Baada ya kipindi cha kwanza kuisha bila ya kupatikana goli, Romelu Lukaku, alifunga goli lake la kwanza katika michuano hiyo kwa kutumbukiza mpira pembeni mwa goli la Jamhuri ya Ireland.

Mchezaji Axel Witsel alifunga goli la pili la Ubelgiji kwa kichwa katika dakika ya 61, kabla ya Romelu Lukaku tena kuachia shuti lililojaa wavuni kufuatia kufanywa shambulizi la kushtukiza.
                           Romelu Lukaku akiachia shuti lililozaa goli la tatu kwa Ubelgiji
                                 Axel Witsel akishangilia goli lake alilofungwa kwa kichwa 
Romelu Lukaku akitokwa na machozi baada ya kufunga goli la kwanza akiwa anashagilia na mdogo wake Jordan

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni