.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Alhamisi, 16 Juni 2016

TANZANIA MWENYEJI MAADHIMISHO YA 6 WIKI YA MAJI BARANI AFRIKA

JIM1Mkurugenzi Msaidizi Maji Shirikishi kutoka Wizara ya Maji na Umwagiliaji Bw. Sylivester Matemu akiongea na waandishi (hayupo pichani) kuhusu Maadhimisho ya 6 ya Wiki ya Maji Barani Afrika na Mkutano wa 10 wa Baraza la Mawaziri wa Maji wa Nchi za Afrika utakaofanyika kuanzia tarehe 18-22 Julai 2016. Kulia ni Afisa Mawasiliano wa Wizara hiyo Bw. Dennis Kiilu.
JIM2Waandishi wa Habari wakifuatilia mkutano huo
 
Frank Mvungi- Maelezo

Tanzania Mwenyeji maadhimisho ya 6 ya wiki ya Maji Barani Afrika na Mkutano wa 10 wa Baraza la Mawaziri wa Maji wa Nchi za Afrika yatakayofanyika Julai,2016 Jijini Dar es salaam.

Kauli hiyo imetolewa na Mkurugenzi Msaidizi Maji Shirikishi kutoka Wizara ya Maji na Umwagiliaji Bw. Sylivester Matemu wakati wa mkutano na waandishi wa Habari leo jijini Dar es salaam.

Mgeni Rasmi katika Ufunguzi wa Maonyesho ya Wiki ya maji yatakayofanyika kabla ya mkutano wa Baraza la Mawaziri atakuwa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Kassim Majaliwa.

Akifafanua Matemu amesema kuwa mkutano huo utahusisha washiriki zaidi ya 1000 kutoka mataifa 54 kutoka Bara la Afrika na wengine kutoka nje ya Afrika.

Maadhimisho hayo yataambatana na maonyesho ya shughuli za wadau wa sekta ya maji na umwagiliaji, kwenye Ukumbi wa Kimataifa wa Mwalimu Nyerere Jijini Dar es salaam.

Kauli mbiu ya kongomanao hilo ni “ Kufikia lengo la maendeleo Endelevu Juu ya usalama wa Maji na usafi wa mazingira” alibainisha Matemu.

Mkutano huo utawasaidia wataalamu wa maji kutoka Mataifa mbalimbali ya Afrika kujadiliana kuhusu mikakati mbalimbali itakayosaidia kupambana na changamoto zinazoikabili sekta ya maji katika bara la Afrika.

Akizungumzia faida za Mkutano huo Matemu amesema kuwa utasaidia kufungua fursa mbalimbali zilizopo katika sekta ya maji na Sekta nyingine ikiwemo kukuza na Kutangaza vivutio vilivyopo hapa nchini hali itakayosaidia kukuza Utalii.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni