.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Alhamisi, 21 Julai 2016

KARIBU MJUMBE: MAKAMU WENYEVITI WA CCM BARA NA ZANZIBAR WAMKARIBISHA MJUMBE WA KAMATI KUU YA CCM, RAIS DKT. MAGUFULI LEO

Makamu Mwenyekiti wa CCM-Bara, Philip Mangula na Makamu Mwenyekiti wa CCM-Zanzibar, Rais Dk. Ali Mohammed Shein, wakimuonyesha kiti cha kukaa, Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM, Rais Dk. John Magufuli, walipoingia ukumbini, kabla ya kuanza Kikao cha Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya CCM, kilichoongozwa na Mwenyekiti wa CCM, Dk Jakaya Kikwete, katika ukumbi wa Sekretarieti, katika jengo la White House, Makao Makuu ya CCM mjini Dodoma, leo.Kamati kuu hiyo ilikuwa ni kwa ajili ya kupendekeza jina la Dkt Magufuli kuwa Mwenyekiti na baadae kuliwasilisha jina hilo kwenye Halmashauri kuu ya Taifa kwa ajili ya kupeleka kwenye mkutano.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni