.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumanne, 26 Julai 2016

KOFFI OLOMIDE AFIKISHWA MAHAKAMANI KINSHASA KWA KUMSHAMBULIA DANSA WAKE WA KIKE

Mwanamuziki nyota wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, Koffi Olomide amefunguliwa shtaka la kushambulia na kumuumiza dansa wake wa kike katika mahakama Jijini Kinshasa.

Mashtaka hayo yamefunguliwa siku tatu kupita tangu atimuliwe Kenya baada ya video ya tukio hilo kusambazwa kwenye mitandao ya jamii akionekana akimpiga teke mwanamke.

Maafisa polisi walimkamata Koffi nyumbani kwake Kinshasa ambapo walimfunga pingu na kisha kuondoka naye kwenye gari lao, ambapo baadaye alifikishwa mahakamani.

Iwapo atatiwa hatiani Koffi Olomide anaweza kufungwa jela miaka mitano. Mwaka 2012 alipewa adhabu wa kifungo cha uangalizi cha miezi mitatu baada ya kumpiga prodyuza wake.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni