.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumapili, 24 Julai 2016

KOFFI OLOMIDE ATIMULIWA KENYA BAADA YA TUKIO LA KUMPIGA TEKE MWANAMKE

Mamlaka za nchini Kenya zimemuondoa kwa nguvu nchini humo mwanamuziki nyota barani Afrika Koffi Olomide baada ya tukio la kumpiga teke dansa wake mwanamke.

Tukio hilo lililonaswa kwenye picha za video Jijini Nairobi katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Jomo Kenyatta, liliibua hasira za wananchi kwenye mitandao ya jamii.

Olomide, anayetokea nchi ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, alikanusha kumshambulia dansa wake saa chache baada ya tukio hilo, hata hivyo alikuja kukamatwa baadae na polisi.

Koffi Olomide aliyekuwa afanye tamasha lake jana Jijini Nairobi, alisafirishwa na kurejeshwa Jijini Kinshasa nchini DRC, akiwa na wachezaji wake shoo watatu.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni