Aidha Katunzi alianisha mambo mbalimbali ikiwa ni pamoja na vyanzo vya mapato vya Mamlaka za serikali za Mitaa, ikiwa ni mapato ya ndani, ruzuku kutoka serikali kuu na Mikopo. Madiwani walifundishwa mbinu za kuongeza mapato ya Hamashauri ambapo walifundishwa namna ya kubuni na kuanzisha vyanzo vipya vya mapato, kuboresha viwango vya tozo, kuboresha mbinu za ukusanyaji mapato, kusimamia matumizi ya fedha za serikali ya mitaa na udhibiti wa fedha za Halmashauri. Source:Father Kidevu Blog,Kagera
Madiwani kutoka Hamashauri za Wilaya ya Kyerwa na Biharamulo wakifuatilia mada hiyo ya Usimamizi na Udhibiti wa fedha za Mamlaka ya Serikali za mitaa.
Wakuu wa Wiaya za Kyerwa na Biharamulo mkoani Kagera, Kanali Mstaafu, Shaabn Lissu (kushoto) wa Kyerwa na Saada Malunde wa Biharamulo wakiwa na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Biharamulo, Wende Ng'ahala (kulia) wakifuatilia mada hiyo.
Ofisa Mipango wa Wilaya ya Biharamulo, Andambike Kyomo akifafanua jambo kuhusu namna ya ugawaji wa fedha za Halmashauri kwa makundi ya Vijana, Wanawake na matumizi mengine.
Mratibu wa Mradi wa PS3 kutoka Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Bertha Swai akifafanua jambo kuhusu mada hiyo na maswali yaliyoulizwa na washiriki.
Ili kuondoa uchovu kwa washiriki kunakosababisha kusinzia wakati wa mafunzo, washiriki walifanya mazoezi kuchangamsha mwili na kuimarisha usikuvu.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni