.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumapili, 24 Julai 2016

MOTO WA NYIKA WALAZIMISHA MAMIA YA WATU KUKIMBIA MAKAZI YAO

Moto mkubwa wa nyika unaosambaa kwa kasi umewalazimisha mamia ya watu kukimbia makazi yao katika eneo la mlimani la kaskazini mwa Los Angeles, California nchini Marekani.

Moto huo umesambaa katika eneo la hekari 20,000 hadi jana usiku, na kusambaza moshi mkubwa katika kaunti ya Los Angeles.

Watu wapatao 300 wameondolewa katika makazi yao karibu na mji wa Santa Clarita, huku mabwawa ya kuogelea ya umma yaliyopo Pasadeana na Glendale yakifungwa kutokana na kuzingirwa na moshi na kujaa majivu.
            Watu wakikimbia kunusuru maisha yao kufuatia kububuka kwa moto huo wa nyika
               Vikosi vya zimamoto vikihaha kukabiliana na moto huo
                        Ndege ikiwa angani ikimwaga kemikali za kuzima moto 

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni