.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumamosi, 16 Julai 2016

RAIS FRANCOIS HOLLANDE KUONGOZA MKUTANO WA DHARULA WA USALAMA

Rais Francois Hollande wa Ufaransa ataongoza mkutano wa kujadili mashambulizi ya kigaidi na waziri wa mambo ya ndani kufuatia shambulizi la Alhamisi Mjini Nice lililouwa watu 84.

Bw. Hollande, ambaye amesema shambulizi hilo ni la kigaidi, tayari ameongeza muda wa hali ya tahadhari katika taifa hilo kwa miezi mitatu.

Alhamisi dereva mwenye lori aliligonga kwa makusudi kundi la watu wakati wa maadhimisho ya Siku ya Bastille katika eneo la ufukweni la Promenade des Anglais.

Polisi walifanikiwa kumuua kwa risasi dereva huyo ambaye ametambulika kuwa ni Mohamed Lahouaiej-Bouhlel, 31, raia wa Tunisia.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni