Timu
ya Wales imejikuta ikishindwa kuweka historia ya kutinga fainali za
michuano ya Euro baada ya kukubali kipigo cha magoli 2-0 kutoka Ureno
katika mchezo uliopigwa huko Lyon.
Katika
mchezo huo washambuliaji nyota wa Real Madrid Cristiano Ronaldo na
Gareth Bale wote walishindwa kutikisa nyavu katika kipindi cha kwanza
kilichoishia bila kufungwa goli.
Hata
hivyo katika kipindi cha pili Ronaldo aliandika goli la kwanza la
mchezo huo kwa mpira wa kichwa katika dakika ya 50, na kuifanya Ureno
iongoze.
Wakati
Wales na Bale wao wakiwa bado wanatafakari goli hilo, Ronaldo tena
aliachia shuti ambalo Luis Nani aliugonga mpira huo na kuandika goli
la pili katika dakika ya 53.
Cristiano Ronaldo akiwa juu angani baada ya kuupiga mpira kwa kichwa ambao unaelekea wavuni
Mpira wa kichwa uliopigwa na Ronaldo ukijaa wavuni na kumshinda kipa wa Wales
Luis Nani akiugonga mpira uliopigwa na Ronaldo na kuubadilisha muelekeo na kuandika goli la pili




Hakuna maoni :
Chapisha Maoni