.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Alhamisi, 7 Julai 2016

RONALDO AIZAMISHA WALES NA KUONYESHA UBORA WAKE DHIDI YA BALE

Timu ya Wales imejikuta ikishindwa kuweka historia ya kutinga fainali za michuano ya Euro baada ya kukubali kipigo cha magoli 2-0 kutoka Ureno katika mchezo uliopigwa huko Lyon.

Katika mchezo huo washambuliaji nyota wa Real Madrid Cristiano Ronaldo na Gareth Bale wote walishindwa kutikisa nyavu katika kipindi cha kwanza kilichoishia bila kufungwa goli.

Hata hivyo katika kipindi cha pili Ronaldo aliandika goli la kwanza la mchezo huo kwa mpira wa kichwa katika dakika ya 50, na kuifanya Ureno iongoze.

Wakati Wales na Bale wao wakiwa bado wanatafakari goli hilo, Ronaldo tena aliachia shuti ambalo Luis Nani aliugonga mpira huo na kuandika goli la pili katika dakika ya 53.
Cristiano Ronaldo akiwa juu angani baada ya kuupiga mpira kwa kichwa ambao unaelekea wavuni
      Mpira wa kichwa uliopigwa na Ronaldo ukijaa wavuni na kumshinda kipa wa Wales
Luis Nani akiugonga mpira uliopigwa na Ronaldo na kuubadilisha muelekeo na kuandika goli la pili


Hakuna maoni :

Chapisha Maoni