.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Ijumaa, 1 Julai 2016

UMOJA WA KIJAMII (UKI) CHUO CHA SMMUCo WATEMBELEA KITUO CHA KULEA WATOTO WENYE MAHITAJI MAALUM CHA KILIMANJARO ORPHANAGE CENTRE

Baadhi ya watoto wanaoishi na kulelewa katika kituo cha Kilimanjaro Orphanage Centre
Wanaumoja wakiwa katika picha ya pamoja katika lango kuu la kuingia chuoni hapo kwa kampasi ya mjini kabla ya kuelekea kituoni
Wana UKI wakikaribishwa na kupewa maelezo ya awali kutoka kwa Mkurugenzi wa kituo hicho Bw.Lazaro Edward mara tu walipowasili
Wana UKI wakicheza na watoto wa Kilimanjaro Orphanage Centre
Watoto wakiteta jambo huku nyuso zao zikiwa na tabasamu la kutembelewa na wageni

Kulia ni mwenyeketi wa UKI Bw. Msiyaki Kuruchumila akikabidhi zawadi kwa watoto hao
Mwenyekiti wa vijana CCM mkoa wa Kilimanjaro Juma Raibu (Kushoto) akiwa na Rais wa Serikali ya wanafunzi SMMUCo Edgar Nziku ambao wote  ni wana UKI wakiwa na watoto kituoni hapo.
 
Umoja wa Kijamii (UKI) ulioanzishwa na wanafunzi wa chuo kikuu cha Stefano Moshi Memorial University wenye lengo la kuitumikia jamii kwa kujitolea kupunguza changamoto za ukali wa maisha katika jamii ulipata fursa ya kukitembelea kituo cha kulea watoto yatima na wenye mahitaji maalum cha Kilimanjaro Orphanage Centre kilichopo kata ya Pasua wilaya ya Moshi mjini  mkoa wa Kilimanjaro.

 Akizungumzia historia yao, Mkurugenzi wa kituo hicho Bw. Lazaro Edward alisema kituo hicho kinachopokea watoto kuanzia umri wa miaka mitatu na kuendelea kwasasa kinalea watoto wapatao 79 huku watano kati yao wakiwa ni waathirika wa virusi vya Ukimwi kueleza kuwa changamoto kubwa inayowakabili ni idadi ya vitanda pamoja udogo wa eneo lakini wanatarajia kukihamisha kituo hicho baada ya ujenzi wa kituo rasmi kukamilika.

Wanaumoja wa UKI wanaosoma kozi mbali mbali walikuwa na wasaha mzuri wa kucheza , kuongea pamoja na kuwakabidhi zawadi watoto hao zenye thamani ya shilingi laki tatu.

 Akieleza lengo la kukitembelea kituo hicho mwenyeketi wa umoja huo Bw. Msiyaki Kuruchumila mwanafunzi wa Elimu na Usimamizi wa Bishara alisema kuwa hii ni sehemu ya muendelezo wa  majukumu yao kama Umoja wa Kijamii na hivyo bado safari yao kuelekea kujitoa kwa jamii bado ni ndefu.

 Mwandishi wetu alipotaka kujua kwanini kuhusu umoja huu kuwa umejikita zaidi katika chuo cha SMMUCo na je yapo malengo zaidi ya kuutanua,Bw. Kuruchumila alisema kuwa wapo katika mchakato wa kuuneza katika vyuo vyote katika mkoa wa Kilimajaro na wanajitahidi hili liwe limekamilika kabla ya mwezi wa kumi na moja mwaka huu. 

"Sisi kama SMMUCo peke yetu hatuwezi kwa kuwa jamii inamahitaji mengi na baada ya kuridhika kuhusu uimara wetu ndani ya SMMUCo tumeanza mchakato kuhakikisha UKI inasambaa katika vyuo vyote hapa Moshi ikiwa ni MOCu, KCMC,MWECAU na MWEKA" alihitimisha.

Akizungumzia ziara hiyo mmoja kati ya wanaumoja huo Godilisten Mnuo alisema kuwa amejifunza mambo mengi hasa upendo kutoka kwa watoto hao na kutoa wito kwa wadau mbali mbali kuwa na tamaduni ya kudumisha uhusiano na wenye mahitaji kwa moyo wa dhati katika jamii ili kwani hii ndio sifa bora machoni pa Mungu na wanadamu.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni