Uturuki
imewashtaki rasmi majenerali 99 kwa kuhusika na mapinduzi yaliyozimwa
ya mwishoni mwa wiki.
Wakati
huo huo rais wa Uturuki Erdogan anakutana na makamanda wa jeshi
watiifu pamoja na baraza lake la mawaziri Jijini Ankara.
Mamlaka
za nchi hiyo zimepiga marufuku kwa wanataaluma kusafiri nje ya nchi,
wakati msako wa watumishi wa umma wanaoshukiwa kuhusika na mapinduzi
hayo ukiendelea.
Zaidi
ya watu 50,000 wamekamatwa, kufukuzwa kazi ama kusimamishwa kazi kwa
kuhusika mapinduzi hayo.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni