Goli la dakika za mwisho la Diego
Costa limempatia kocha Antonio Conte ushindi usiotarajiwa akiwa
Meneja wa Chelsea wakati wa mchezo wao wa kwanza wa Ligi Kuu ya
Uingereza dhidi ya West Ham.
Mshambuliaji huyo wa raia wa
Hispania alifunga kwa shuti la umbali wa yadi 20 katika dakika ya 89,
na kuwafanya mashabiki wa Chelsea wapagawe katika dimba la Stamford
Bridge, huku Conte akiungana nao.
Katika mchezo huo ulioishia kwa
ushindi wa magoli 2-1, Eden Hazard alikuwa wa kwanza kuifungia
Chelsea kwa mkwaju wa mpira wa adhabu baada ya Michail Antonio
kumfanyia madhambi Cesar Azpilicueta. Hata hivyo James Collins
aliisawazishia West Ham.
Diego Costa alikuwa na bahati kutopewa kadi nyekundu kwa kumfanyia madhambi kipa Adrian
Adrian akiugulia maumivu huku akimuonyesha Diego Costa namna alivyomuumiza na kumsababishia jeraha
Eden Hazard akiachia shuti lililojaa wavuni na kuiandikia Chelsea goli la kwanza




Hakuna maoni :
Chapisha Maoni