.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Alhamisi, 25 Agosti 2016

JOTO LAWAATHIRI SENENE NCHINI UINGEREZA

Imebainika kuwa senene, hawa senene wadudu jamii ya panzi, wanasumbuliwa na joto kiasi cha miili yao kuwa na rangi ya pinki kama rangi ya ngozi ya mzungu aliyechomwa sana na jua, wenyewe wanaita sunburn.
 

Hilo limebainika katika utafiti ulioendeshwa kwenye hifadhi ya misitu na miti huko Suffolk, nchini Uingereza, ambao umebaini pia joto huwafanya senene washindwe kuruka na kuzubaa tu katika majani.
 

Kabla ya kufanyika kwa utafiti huo, wanandoa wawili wa eneo hilo waliokuwa wamepumzika ufukweni kwa ajili ya kuota jua, walimuona senene mmoja akiwa amezubaa majanini huku mwili wake ukibadirika rangi na kuwa wa pinki
Wanandoa hao walimchukua senene huyo na kumpeleka katika taasisi moja ya utafiti wa wadudu na ndipo utafiti wa awali ulionyesha kuwa senene nao husumbuliwa na joto na miili yao hubadilika rangi na kuchoka wanapopigwa na jua kali au kupata joto kali.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni