.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumatatu, 22 Agosti 2016

MICHUANO YA OLIMPIKI RIO 2016 YAFUNGWA KWA SHAMRASHAMRA


Rio imemaliza michuano ya Olimpiki kwa shamrashamra za aina yake, licha ya mvua kuwanyeshea maelfu wanamichezo pamoja na watazamaji waliofika kushuhudia michezo hiyo kutoka maeneo mbalimbali duniani.

Mwenge wa Olimpiki umezimwa katika uwanja wa Maracana nchini Brazil, na kuashiria michuano ya Olimpiki Rio imemalizika rasmi.

Gavana mpya wa Tokyo, Yuriko Koike, ambaye ni mwanamke wa kwanza kushika wadhifa huo alipokea bendera ya Olimpiki kutoka kwa Meya wa Rio, Eduardo Paes, ikiwa ni kuipokeza Japan jukumu la kuandaa michuano ijayo ya Olimpiki.
   Mwanga wa fataki zilizotumika katika kupamba sherehe hizo ukioneka kwa juu ya uwanja
                        Shamrashamra zikiendelea ndani ya uwanja kama inavyoonekana 
 Watumbuizaji wakitumbuiza kwa furaha wakati wa sherehe za kufungwa michuano ya Olimpiki Rio 2016


Hakuna maoni :

Chapisha Maoni