.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumamosi, 20 Agosti 2016

MTU MZIMA ZLATAN IBRAHIMOVIC ASHIKIKI LIGI KUU YA UINGEREZA

Zlatan Ibrahimovic ametikisa nyavu mara mbili na kuipa ushindi wa nyumbani Manchester United wa magoli mawili kwa bila dhidi ya Southampton katika mchezo wa Ligi Kuu ya Uingereza.

Mshambuliaji huyo hatari raia wa Sweden aliwanyanyua mashabiki wa Manchester United katika dimba la Old Trafford baada ya kuupiga kichwa mpira wa krosi iliyopigwa na Wayne Rooney na kuandika goli la kwanza.

Ibrahimovic alifunga goli la pili kwa mkwaju wa penati baada ya Jordy Clasie kumuangusha beki wa Manchester United Luke Shaw. Paul Pogba aliyevunja rekodi ya uhamisho wa paundi milioni 89 alicheza kwa mara ya kwanza na kuonyesha uwezo wake.
Ibrahimovic na Paul Pogba wakiangalia mpira wa kichwa ukielekea wavuni na kuipatia Manchester United goli la kwanza
 Zlatan Ibrahimovic akijipinda kuachia shuti la mpira wa penati uliojaa wavuni na kuandika goli la pili

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni